DONDOO
ZA MUHIMU KATIKA NDOA!
Nina
kila sababu ya kumshukuru Muumba wangu kwakuwa ni yeye ndiye mlinzi na kiongozi
wa maisha yangu, naamini bila yeye mimi na wewe tusingekuwepo hivyo basi tuna
wajibu wa kumshukuru kila wakati. bila shaka kwa nguvu zake yeye aliye juu
utakuwa mzima wa sifa njema na macho na akili yako vimejiandaa kupata darasa
hili murua la maisha.
Leo
nitazungumza moja kwa moja na wanandoa. Nitazungumza juu ya jambo muhimu sana,
nazungumzia unyenyekevu na uvumilivu katika ndoa bila kujali jinsia, je ni
utumwa? Hapa kila mmoja atakuwa na jibu lake, lakini leo nataka kuwapa ukweli
wa kitaalamu. Kuna usemi usemao ukitaka kujua uhondo wa ngoma uingie ucheze,
wengine pia husema ukitaka kujua utamu na uchungu wa ndoa basi uwe mwanandoa,
usemi huu una kweli ndani yake, wewe ambaye hujaingia kwenye ndoa naamini si
rahisi kujua shida ama starehe apatazo mume ama mke ndani ya ndoa, pengine kama
utazijua ni kwa kuzisikia kwa wanandoa ambao wanaeleza maisha yao. Hata kama
utayasikia hutajua ukweli yampatayo mwenzio mpaka yakukute mwenyewe kwani mengi
huwa ya siri za ndoa.
Kuna
matatizo mengi wapatayo wanandoa, ukiniambia nitaje matatizo yaliyopo katika
ndoa za watu nitaeleza mengi sana kutokana na uzoefu wangu pamoja na tafiti
mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa mambo ya mapenzi.
Lakini
wakati nikizitaja kero za ndoa pia kuna upande wa pili ambao ni furaha, pia
kuna mengi mazuri wayapatayo wanandoa wanakuwa katika ndoa zao.
MAANA
YA NDOA
Ndoa
ina maana kubwa sana katika maisha ya binadamu, hata hivyo ina tafsiri nyingi
kulingana na imani au mahali ndoa ilipofungwa! Kwa Wanasaikolojia ya Mapenzi
ndoa ni ukamilifu wa makubaliano ya muungano wa mwanamke na mwanaume wenye
kupendana kwa lengo la kuishi pamoja kama mume na mke kulingana na sheria ya
dini, mila au desturi za sehemu fulani.
Pamoja
na tafsiri hiyo ambayo hutambuliwa na wataalamu wa mambo ya mapenzi, hawashauri
wanandoa kuachana, maana kama waliungana kwa upendo basi wan apaswa kuishi kwa
upendo na kusikilizana siku zote, huo ndiyo upendo wa kweli ambao
Wanasaikolojia wa Mapenzi wanatambua.
ULINZI
WA NDOA
Hapa
ndipo kwenye msingi wa mada yetu, unapoingia kwenye ndoa kitu cha kwanza
unatakiwa kufikiria jinsi ya kuilinda ndoa hiyo kwa gharama yoyote! Kuingia
kwenye ndoa na kutoka baada ya muda mfupi ni kujitafutia laana ambayo haina
ulazima wowote, hapa unatakiwa kufikiria mpaka mwisho wa uwezo wa kufikiri ili
ndoa yako idumu na usije ukajikuta umeingia katika laana hiyo.
Linapokuja
sasa suala la ulinzi wa ndoa yako, utashindwa kumnyenyekea mpenzi wako?
Unatashindwa kumvumilia mpenzi wako kwa sababu utajihisi wewe ni mtumwa wa
mapenzi? Wapi imeandikwa hii? Mathalani mkeo anaumwa na kwa bahati mbaya hamna
msichana wa kazi, je utashindwa kumsaidia kazi kama kupika, kufua, kuosha
vyombo na kazi nyinginezo kwasababu tu, wewe ni mwananume? Haingii akilini hata
kidogo.
UVUMILIVU...
Katika
maisha anayohitaji kuyavumilia mwanadamu ni maisha ya ndoa. Ndoa inakuwa na
mambo mengi sana, kutunza familia, kupeana haki za nyumba, kusaidiana na
kuvumiliana katika vipindi vya dhiki na faraja na mengineyo. Ukarimu, uaminifu,
upendo wa kweli ni kati ya chachu za kudumisha penzi na kamwe halitaweza
kuchuja.
Unapooa
au kuolewa lazima ufahamu kuwa unakuwa umejenga undugu baina ya familia yako na
ya mwenzio. Katika kuishi kwenu huko utakutana na matabaka mengi, watu
hutofautiana tabia, mfano wewe mwanamke umeolewa, mumeo akaleta ndugu, yaani
wifi zako.Unatakiwa kuwasoma wifi zako tabia ili uweze kuendana nao, ili
kufanikiwa unapaswa uwe na busara, mvumilivu, mnyenyekevu, na kuonyesha
kuwajali, hii inaweza kukusaidia sana kwani watakapokutendea mambo ya ajabu
nawe ukaanza kuwaropokea matusi, utakuwa unajingiza kwenye migogoro ambayo
mwisho wake huweza kuwa mbaya zaidi kwako kuliko kwao.
Kumbuka
kuwa Mungu ametuumba kila mtu na udhaifu wake, ndio maana unaona wanandoa wengi
wanajikuta wakizikimbia ndoa zao kwa kutendwa na wandani ama ndugu wa wandani
wao, wakati mwingine mume anaweza kuwa hajui, unayepaswa kumweleza ni wewe, na
unapomweleza lazima uzingatie heshima na busara ambayo haitaonyesha kwamba umedharau
ukoo wao.
Sio
unaanza kusema; "Nyoo! Umeniletea ukoo wenu hapa, chakula hakitoshi!
Nitawafukuza!" Kwa kauli hiyo utaonekana limbukeni, kaa naye chini zungumza
naye kwa ukarimu mweleze ni jambo gani linalokunyima uhuru wewe kama mkewe wa
ndoa. Usimfiche, mwambie; "Mume wangu, kuna jambo wifi amenitendea sijui
kama anaona ni kosa lakini mie naona amenikosea, mweleze asirudie tena,"
tena hakikisha wakati unamweleza haya mpo peke yenu chumbani na huenda ni baada
ya kumpa haki yake. Upo hapo?
Huo
ndiyo uvumilivu ninaouzungumzia, siku zote wewe ndiye unayetakiwa kuwa na
uchungu na ndoa yako. Kabla ya kuzungumza jambo lolote fikiria mara mbili,
halitasababisha matatizo kwako? Ukipata matatizo au kuachika huyo wifi yako
atakuwepo? Jibu ni hapana! Utakaporudishwa nyumbani kwenu, utawaangaliaje
wazazi wako ambao walikulea katika malezi mazuri na kukufunda vyema? Ni nini
kama siyo aibu mtoto wa kike utakuwa umewapelekea wazee wako?
Kaa
chini, fikiria kwa makini kabla ya kuamua jambo lolote linalohisu ndoa yako.
Kumbuka kuwa kuingia kwenye ndoa ni kazi ngumu lakini kazi ngumu zaidi ni
kuhakikisha unailinda ndoa yako inaendelea kuwa hai siku zote, ndiyo kusema
kwamba siku mnasherehekea miaka 10 au jubilee ya ndoa yenu utakuwa ukijimiminia
misifa kibao kibao kuwa kama siyo uvumilivu wako usingeweza kufikia hatua hiyo.
UNYENYEKEVU
JE?
Sawa
kabisa! Sasa kama usipomnyenyekea lahazizi wako, ambaye mwenyewe ulikubali kuwa
naye na kufunga naye ndoa unataka umnyenyekee nani? Mumeo/mkeo ndiyo wa
kumnyenyekea siku zote za uhai wako. Lazima uwe na kauli ya upo iliyojaa
ukaribu. Ndoa kubembelezana bwana, mpenzio akija na mawazo yake, mtu amemuudhi
kazini kwako ndio mahali haswa anapopaswa kunyenyekewa na kupewa raha.
Wewe
ndiye unapaswa kumsahaulisha kabisa mambo yote yaliyotokea kazini. Mpokee kwa upole,
mwambie poile, mkaribishe chumbani kisha mvue nguo zake na umpeleke bafuni
mwenyewe. Anza kumwogesha bila kuzungumza naye maneno mengi. Tumia dodoki au
kitambaa laini kumsafisha ngozi ya mwili wake.
Baada
ya hapo mkaushe kwa taulo laini kisha mrudishe chumbani, mtolee nguo za usiku
kisha mpeleke mezani kwa chakula. Baada ya hapo sasa mkiwa sebuleni mnaangalia
tamthiliya mwulize kwa upole huku macho yakiwa yanazungumzia mapenzi. “Darling
vipi, mbona leo naona sio kawaida yako? Umechokachoka...kuna nini mpenzi wangu
jamani?” Amini nakuambia kwa kauli kama hiyo hata kama alikuwa na tatizo kubwa
anaweza akakujibu; “Ah kuna mtu aliniudhi kidogo ofisini, lakini baada ya
kufika hapa nyumbani najisikia amani sasa,” tena wakati anakuambia hivi ujue
lazima atakuwa anaachia tabasamu mwanana sana.
Nikufundishe
tena hapo cha kufanya? Mh! Unamsogelea kisha unabusu halafu unapima joto la
homa yake ya mapenzi, kama limepanda mshike mkono mwahishe chumba cha upasuaji
kabla hujampoteza mtoto wa mwanamke mwenzio.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni