Assalaam alaykum Warahamtullahi Wabarakatuh.
Misingi au njia ya kuamiliana na watu, tunayapata katika wasia wa Allah uliokuja katika Qur'an ndani ya Surat Alhujurat, uzingatieni.
1⃣
unapoletewa khabari yoyote basi kwanza unatakiwa uichunguze kwanza ili
ujue uhakika na ukweli wake, ili usije kulihukumu jambo kimakosa ukaja
ukajuta baadae, hali ya kuwa majuto yatakuwa mjukuu muda huo.
2⃣
Pindi ukitokea ugomvi baina ya Waislamu wawili, au makundi mawili, Basi
Allah mtukufu anatuusia kusuluhishana na kupatanishana, kwa kutumia
kila njia ya kidiplomasia kufikia lengo, na si kukaa kufurahia na
kuchochea ugomvi, hii si tabia ya Muumini.
3⃣ Pia Allah mtukufu anatuusia kuwa waadilifu na kutenda haki tunapotoa hukumu, na si kumpa haki mmoja na kumdhulumu mwengine.
NB: Haki na uadilifu unaingia pia katika Mizani hasa katika nyanja za Biashara, wauzaji wawe waadilifu na wajitahidi kadri wanavyoweza kutowadhumu wateja wanapowapimia bidhaa.
Na wale wahusika wa Mizani katika ofisi za kununua Karafuu, Mwani, Pamba nk, wawe waadilifu na watenda haki katika Mizani, Allah ametoa onyo kali juu ya hili.
4⃣
Allah mtukufu pia anatuusia kuhusu suala zima la kutofanyiana mizaha
mikubwa na suala zima la kudharauliana na kubaguana, kwani huwenda huyo
unayemdharau akawa ni bora mbele ya Allah mtukufu, hata akawa
maskini,mnyonge, dhaifu, kabila yake si tukufu/kubwa, rangi yake,cheo
chake na mambo yanayofanana na hayo, wanaadamu sote ni sawa tofauti za
kimaumbile tulizonazo ni mwenyewe Allah andiye aliyetaka hivyo, na hii
yote ni kuonesha uwezo wake na fani yake katika kuumba.
5⃣
Allah pia anatuusia kutovunjiana heshima, sisi sote ni wakarimu Allah
ametutukuza na kutufanya kuwa viumbe bora kuliko wengine ulimwenguni,
kwa hivyo kila mmoja anatakiwa kumuheshimu mwenzake na kuheshimu mawazo
na maamuzi yake.
6⃣
Allah mtukufu anatuusia kuacha kuitana kwa majina mabaya na
kuchokozana, hiyo ni tabia ya watu mafasiki, sisi Waumini haifai kufanya
hivyo, tuitane kwa majina yaliyo mazuri, yenye maana nzuri,
yanafurahisha mioyo yetu, na wasia huu pia kwa wazazi Allah
anapowaruzuku watoto wawape watoto wao majina mazuri kama majina ya
Masahaba na mitume na watu wema.
7⃣
Allah mtukufu anatuusia tuache tabia ya kudhaniana vibaya, kwani hakika
ya dhana ni uovu/dhambi, tunatakiwa siku zote tuwe na dhana nzuri kwa
wenzetu huo ndio uislamu.
8⃣
Pia Allah mtukufu anatuasa kuacha tabia ya kuchunguzana, kufuatiliana
na kupelelezana, si tabia nzuri kuchunguza aibu za mwenzako, na muislam
aliye bora ni yule anayejiweka mbali na mambo yasiomuhusu, kufanya hivyo
ni kujiweka mbali na matatizo.
9⃣
Allah mtukufu anatuusia pia kuacha tabia ya kusemana vibaya nyuma ya
pazia na kusengenyana, kufanya hivyo ni sawa na kula nyama ya ndugu yako
unayemsengenya anapokuwa maiti.
Haya yote Allah mtukufu anatuusia kuachana nayo, kufanya hivyo ndio tutasalimika hapa duniani kwa kuishi maisha ya furaha na kusalimika huko Akhera tunakokwenda.
Tafadhali watumie na wengine nao waujue wasia wa Allah uliokuja ndani ya Surat Alhujurat.
Kama kuna kosa rekebisha, Allah anajua zaidi.
Abuu Zahrah Masoud Al-Bimani.
Misingi au njia ya kuamiliana na watu, tunayapata katika wasia wa Allah uliokuja katika Qur'an ndani ya Surat Alhujurat, uzingatieni.
NB: Haki na uadilifu unaingia pia katika Mizani hasa katika nyanja za Biashara, wauzaji wawe waadilifu na wajitahidi kadri wanavyoweza kutowadhumu wateja wanapowapimia bidhaa.
Na wale wahusika wa Mizani katika ofisi za kununua Karafuu, Mwani, Pamba nk, wawe waadilifu na watenda haki katika Mizani, Allah ametoa onyo kali juu ya hili.
Haya yote Allah mtukufu anatuusia kuachana nayo, kufanya hivyo ndio tutasalimika hapa duniani kwa kuishi maisha ya furaha na kusalimika huko Akhera tunakokwenda.
Tafadhali watumie na wengine nao waujue wasia wa Allah uliokuja ndani ya Surat Alhujurat.
Kama kuna kosa rekebisha, Allah anajua zaidi.
Abuu Zahrah Masoud Al-Bimani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni